MKUU wa wilaya ya Handeni
Muhingo Rweyemamu pamoja na mwanachama wa klabu ya Yanga Abdallah Binkleb jana wamechukua
fomu ya kuwania nafasi ya ujumbe katika uchaguzi wa klabu ya Yanga uliopangwa
kufanyika Julai 15.
Katibu wa kamati ya uchaguzi
ya Yanga Francis Kaswahili ameiambia mamapipiro blog kwamba jana
kwamba wanachama hao wanafanya idadi ya wagombea waliochukua fomu za kuwania
nafsi mbalimbali za uongozi katika klabu hiyo kufikia 10 .
Mbali na hao wanachama
wengine waliochukua fomu ni pamoja na John Jambele anayewania uenyekiti, huku
Ayoub Nyenzi akiwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti.
“Waliochukua fomu kuwania
ujumbe wa kamati ya Utendaji mbali na Muhingo na Binkleb ni Isack Chandi, Jumanne Mwamwenye na Salehe Hassan,”alisema.
Comments
Post a Comment