Kocha mkuu wa Simba Milovan Cirkovic ataanza kukinoa kikosi chake kesho kwenye viwanja vya TCC Chang'ombe.
Aidha, kocha
huyo anatarajiwa kusaini mkataba mpya wa kukinoa kikosi hicho wakati wowote.
Milovan
ambaye alikuwa kwao Serbia kwa mapumziko, aliwasili usiku wa kuamkia leo.
Wachezaji
wa Simba walianza kujinoa mapema mwezi huu kwa kufanya mazoezi ya kujenga mwili
‘Gym’ kabla ya kuhamia uwanjani hivi karibuni ikiwa ni sehemu ya maandalizi yao
ya michuano ya kombe la kagame linalotarajiwa kuanza juni 14 jijini Dar es
Salaam.
Ofisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga
alisema kwamba Milovan ataanza kazi yake hiyo ambayo ilikuwa chini ya kocha
msaidizi Richard Amatre na kocha wa timu ya vijana Amri Saidi.
Alisema
kikosi cha Simba kilichokuwa kanda ya Ziwa kwa ziara maalum kilitarajiwa
kuwasili usiku wa leo ambapo wachezaji wachezaji wake wataanza mazoezi jioni
ya kesho.
Kamwaga
alioongeza kuwa mazoezi hayo pia yatahusisha nyota wake waadamizi wanaokipiga
katika timu ya Taifa wakiwemo Juma Kaseja, Haruna Moshi ‘Boban’, Mwinyi
Kazimoto na Amir Maftah ambao walipewa mapumziko ya wiki moja.
Comments
Post a Comment