TWIGA STARS YAPIGWA 5-2

Kikosi cha Twiga Stars..
TIMU ya taifa ya soka ya wanawake ya Afrika Kusini, Banyana Banyana, jioni hii imeitandiika Tanzania, Twiga Stars mabao 5-2 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.
Hicho ni kipigo cha pili mfululizo kwa Twiga Stars inayonolewa na Nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya wanaume, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa, baada ya wiki iliyopita kufungwa 4-1 na Zimbabwe kwenye Uwanja huo huo katika mchezo wa kirafriki pia.
Aidha, haya ni matunda ya programu mbovu ya maandalizi ya timu hiyo hivi sasa, ambayo mara kwa mara imekuwa ikicheza mechi za kirafiki na timu ya waigizaji, badala ya kuwekeza kwenye maandalizi thabiti ya kuijenga timu.
Katika mchezo wa leo, mabao ya Banyana yalitupiwa nyavuni na Portia Modise dakika ya 23 na 46, Sanah Mollo dakika ya 73 na 79 na Jamine van Wyk dakika ya 86, wakati ya Twiga yalifungwa na Fatuma Bashir dakika ya 67 na Asha Rashid ‘Mwalala’ dakika ya 77. 


Comments