TWIGA STARS YALALA 2-1

Twiga Stars

TIMU ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, imeanza ‘vibaya kidodo’ kampeni za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa kwa wanawake, baada ya kufungwa mabao 2-1 jioni hii mjini Addis Ababa na wenyeji, Ethiopia.
Twiga sasa inahitaji ushindi wa 1-0, Juni 16, katika mchezo wa marudiano mjini Dar es Salaam, ili kukata tiketi ya kucheza fainali hizo kwa mara ya pili mfululizo, Novemba mwaka huu, Equatorial Guinea, zikiwa ni za nane katika historia ya michuano hiyo

Comments