TUZO ZA WANAMICHEZO BORA 2011 MAMBO YAANZA

 


CHAMA Cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimeanza mchakato wa Tuzo kwa Wanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2011.
Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando (pichani kushoto) ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba kama ilivyokuwa mwaka uliopita Kamati ya Utendaji ya TASWA imeamua suala la mchakato wa kuwapata wanamichezo hao lifanywe na kamati maalum nje ya Kamati ya Utendaji ya TASWA lengo ikiwa ni kupanua wigo na kuwashirikisha wadau wengi zaidi katika jambo hili nyeti.
Kutokana na hali hiyo Kamati ya Utendaji ya TASWA imeshateua kamati maalum ya kusimamia tuzo hiyo, ambapo kamati hiyo ambayo tayari imeshaanza vikao vyake jijini Dar es Salaam ipo chini ya Mhariri Mkuu wa gazeti la Spoti Starehe, Masoud Sanani, ambaye pia aliiongoza kamati hiyo mwaka uliopita.
Kamati hiyo ya Tuzo ilikutana mara ya mwisho hivi karibuni kwa ajili ya kupanga namna ya kuendesha tuzo hizo kwa mwaka huu ili iwe bora zaidi ya ilivyokuwa mwaka jana.
Pamoja na mambo mengine kamati ilikubaliana vyama vya michezo vishirikishwe kwa kuviandikia barua ili vitume majina ya wanamichezo wao waliofanya vizuri kwa mwaka 2011.
Kutokana na hali hiyo kila chama cha michezo kitawasilisha  kwa kamati majina matatu ya wanamichezo wake waliofanya vizuri mwaka jana kwa wanaume matatu na wanawake matatu, ambao mmojawao atakuwa ndiye mshindi wa mchezo husika kwa mwaka jana.
Pia kila mshindi miongoni mwa wanamichezo hao atashiriki kuwania tuzo ya Mwanamichezo wa Bora wa Mwaka 2011. Tarehe na mahali ambapo tuzo itafanyika itatangazwa wiki hii baada ya kumalizika vikao muhimu, ambapo pia mdhamini wa tuzo atatajwa, ingawa TASWA inafungua mlango kwa kampuni zaidi zijitokeze kudhamini kwa vile tuzo ya mwaka huu itakuwa ya aina yake.
Kwa hiyo wafuatao ndio wanaunda Kamati ya TASWA ya Kusimamia Upatikanaji wa Wanamichezo Bora wa Tanzania kwa mwaka 2011, wengi wakiwa ni wale waliokuwepo mwaka uliopita..
Mwenyekiti wa Kamati atakuwa Sanan, ambaye ni Mhariri wa gazeti la Spotistarehe, Katibu wa kamati atakuwa Amir Mhando ambaye ni Katibu Mkuu wa TASWA,  Mshauri wa Kamati atakuwa Juliana Yassoda ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo. Pia Kamati itaomba Ofisa mmoja wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) naye kuwa mshauri wa kamati.

Orodha kamili ya wajumbe ni
1.Amour Hassan-Mhariri Nipashe
2. Rashid Zahoro-Mhariri gazeti la Burudani
3. Alex Luambano-Clouds FM
4. Tulo Chambo-Mhariri Tanzania Daima
5. Mbonile Burton-HabariLeo
6. Chacha Maginga-TBC1
7.Frank Sanga-Mhariri Mwanaspoti
8. Michael Maurus-Super Star
9. James Range-Star TV
10.Editha Mayemba-Radio Tumaini
11. Said Kilumanga-Chanel Ten/Magic Radio
12.Rehule Nyaulawa-Mkurugenzi Times FM
13. Angel Akilimali-Meneja Vipindi Radio Uhuru
14. Masoud Sanan-Mhariri Spotistarehe
15. Amir Mhando-Katibu Mkuu TASWA
16. George John –Katibu Msiadizi TASWA
17.Patrick Nyembela-EATV
18: Juliana Yassoda-Naibu Mkurugenzi Idara ya Michezo
19. Luqman Maloto-Championi
20. Deo Rweyunga-Radio One
21. Andrew Kingamkono-Mhariri Mwananchi
22. Dominick Isiji-The African
23. Ofisa kutoka BMT

WAFUNGAJI WA MABAO LIGI KUU BARA


NOJNOGOAL SCORERSGOALSTEAMHTRPNT
119JOHN BOCCO17AZAM FC02
226KENNETH ASAMOAH10YANGA SC00
325EMMANUEL OKWI10SIMBA SC00
420HAMIS KIIZA10YANGA SC01
53NSA JOB 10VILLA SQUAD FC02
630PATRICK MAFISANGO10SIMBA SC01
729SAID BAHANUZI7MTIBWA SUGAR00
827MOHAMED KIJUSO7VILLA SQUAD FC / RUVU SHOOTING02
911GAUDENCE MWAIKIMBA6MORO UNITED00
109JUMA SEMSUE6POLISI DODOMA FC10
1116MRISHO NGASA6AZAM FC00
1228DAVIES MWAPE6YANGA SC00
1310KIPRE TCHETCHE6AZAM FC00
1410FELIX SUNZU6SIMBA SC01

MSIMAMO WA LIGI KUU BARA


NOTEAMSPWDLGFGAGDPTS
1SIMBA SC25185242123059
2AZAM FC25165438132553
3YANGA  SC25154641251649
4MTIBWA SUGAR SC2511683528739
5COASTAL UNION SC25113112629-336
6JKT OLJORO FC259791925-634
7KAGERA SUGAR FC2571172524132
8RUVU STARS SC2571172632-632
9RUVU SHOOTING FC2571082221131
10TOTO AFRICAN FC2551192429-526
11AFRICAN LYON FC2559112129-824
12VILLA SQUAD FC2565142848-2023
13POLISI DODOMA FC2539131833-1518
14MORO UNITED FC2539132744-1718
TOTAL1756253613923920474

SATURDAY, MAY 5, 2012

MAYWEATHER AMTWANGA COTTO, LAKINI AMWAGA MCHUZI

US Boxer Floyd Mayweather (R) Fights
Mayweather kulia akiadhibiwa huku damu zikimtoka puani

US Boxer Floyd Mayweather (R) Fights
Getty Images
2012-05-05
Floyd Mayweather (kulia). 
LAS VEGAS, Marekani
BONDIA Floyd Mayweather Jr. ameendeleza ubabe baada ya alfajir hii kumtandika kwa pointi Miguel Cotto katika pambano lililokuwa kali na la kusisimua.
Mayweather alitumia kasi yake na ufundi kumshinda Cotto, ingawa haikuwa kazi nyepesi kwani mpinzani wake huyo alikuwa akitupa makonde ya maana na kushambulia mwanzo mwisho.
''Wewe ni bingwa hatari,'' Mayweather alimuambia Cotto ulingoni baada ya pambano. 'Wewe ni kinana wa nguvu ambaye sijawhai kukutana naye.''
Mayweather alitawala raundi ya mwisho, ya 12 akimnyanyasa Cotto na kujihakikishia kucheza mapambano 43 bila kupigwa. Tofauti na mapmabano yake mengi, Mayweather alitokwa damu puani mbele ya Cotto.
Majaji wawili walitoa pointi 117-111 na wa tatu akatoa 118-110, hivyo Mayweather ameshinda kwa pointi 116-112.
Mayweather aliyepigana wiki chache tu kabla ya kuingia jela ya kutumikia kifungo cha miezi mitatu, alikutana na pambano gumu dhidi ya mplnzani ambaye anakwenda mbele wakati wote
Lakini alikuwa mwenye kasi na mjanja zaidi ya Cotto na alionekana kumvaa katika raundi za mwisho.
Katika raundi ya mwisho, Mayweather alipiga ngumi yake bora zaidi kwenye pambano hilo, uppercut ya mkono wa kushoto ambayo ilimuonekana kumuumiza Cotto. 
Mayweather, aliyeahidiwa kupewa dola za Kimarekani Milioni 32, alilazimika kupigana kila dakika katika raundi 12 za pambano dhidi ya mbabe huyo wa Puerto Rico. 
Mayweather atakuwa jela wakati Manny Pacquiao anapanda ulingo huo huo wa MGM Grand Juni 9, dhidi ya Timothy Bradley. Pambano tamu zaidi la ngumi wanalolisubir9ia wapenzi wengi wa mchezo huo duniani ni kati ya Mayweather dhidi ya Pacquiao, ambalo halijapangwa kufanyika.
Hii inatokana na msistizo wa Mayweather kutaka Pacquiao afanyiwe vipimo vya kutumia dawa za kuongeza nguvu, ingawa tayari Pacquiao amesema yuko tayari kufanya hivyo.
''Nataka kupigana na Pacquiao, lakini anahitaji kufanyiwa kwanza vipimo vya kutumia dawa za kuongeza nguvu kabla ya kupambana naye,'' alisema Mayweather.
Takwimu za makonde, zinaonyesha Mayweather alipiga ngumi 179 zilizofika kati ya 687 alizotupa na Cotto alipiga ngumi 105 zilizofika kati ya 506.
Cotto, ambaye sasa anakuwa amepigwa mapambano matatu 37, aliahidiwa kupewa dau kubwa zaidi katika historia yake ya kupigana, dola Milioni 8.
US Boxer Floyd Mayweather (L) Fights

Comments