TIBAIGANA KUTOA MAAMUZI MAZITO KESHO


Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inatarajia kukutana Mei 2 mwaka huu kujadili rufani iliyowasilishwa mbele yake na klabu ya African Lyon. 
Klabu hiyo ya Ligi Kuu inailalamikia TFF ikipinga uamuzi uliofanywa na Kamati yake ya Ligi juu ya kuvunjika kwa pambano la ligi hiyo kati ya Azam na Mtibwa Sugar lililochezwa hivi karibuni kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam. 
Katika rufani yake, Lyon imedai uamuzi uliofanywa na Kamati ya Ligi ya TFF haikuwa sahihi, kwani haukuzingatia kanuni za ligi hiyo kuhusu timu inayogomea mchezo. 
Kamati hiyo chini ya Kamishna Mstaafu wa Polisi, Alfred Tibaigana inatarajia kufanya kikao chake kuanzia 8 mchana.

Comments