TFF NAO WAOMBOLEZA KIFO CHA MPENDWA WETU RACHEL MWILIGWA

Marehemu rachet katikati enzi za uhai wake akiwa pamoja na waansioshi wenzake Asha Kigundula kushoto na mdau mwingine katika moja ya mikutano ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) katika ukumbi wa Manispaa ya Kinondoni. Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha Mhariri wa Michezo wa gazeti la Mtanzania, Rachel Mwiligwa kilichotokea leo (Mei 11 mwaka huu) katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam. Msiba huo ni mkubwa katika sekta ya habari na mpira wa miguu kwani Rachel kwa kipindi chote akiwa mwandishi na baadaye Mhariri alikuwa akifanya kazi nasi, hivyo mchango wake katika mpira wa miguu tutaukumbuka daima. TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Rachel, kampuni ya New Habari ambayo ndiyo inayomiliki gazeti za Mtanzania na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito. Mungu aiweke roho ya marehemu Rachel mahali pema peponi. Amina

Comments

Post a Comment