ROMA MKATOLIKI AFUNIKA MBEYA

 

 Roma Mkatoliki akitumbuiza jukwaani wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award jijini Mbeya katika Uwanja wa Sokoine jana.Picha zote naFather Kidevu Blog
 Suma Lee nae alishambulia jukwaa vilivyo na kuleta raha kwa mashabiki katika wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music jijini Mbeya
 Ben Paul nae alishambulia jukwaa vilivyo na kuletya raha kwa mashabiki katika wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award jijini Mbeya.
 Barnaba Boy ambaye ni mshindi wa Tuzo ya Mwimbaji Bora wa Kiume akimbo jukwaani hii leo wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award jijini Mbeya katika Uwanja wa Sokoine
 Vijana wengi walikuwa wamepigilia vitu vya namna hii
 Mashabiki walikuwa hawatulii
Mkali wa Bongo fleva Ali Kiba  akiimba jukwaani hii wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award iliyofanyika uwanja wa Sokoine 
 Wasichana waliokuwa wakitoa huduma ya tiketi
 Mkali wa Bongo fleva Ali Kiba akiimba na Omy Dimpoz katika wimbo Nai Nai akiimba jukwaani hii wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award iliyofanyika uwanja wa Sokoine.Picha zote na Father Kidevu Blog
Dimpoz kwa Pozi akipitika katikati ya wacheza show wake.
 Msanii AT kutoka Zanzibar akitumbuiza jukwaani na wacheza sho wake wakati wa show maalum ya Washindi wa Kili Music Award  jijini Mbeya katika Uwanja wa Sokoine jana
Na  Father Kidevu Blog, Mbeya.
MANENO ya Injili yanayosema wa mwisho anakuwa wa kwanza na wa kwanza anakuwa wa mwisho yametima jana katika Uwanja wa Sokoine Mjini Mbeya pale mkali wa Hip Hop,  Roma  Mkatoliki alipoongoza jahazi la wakali wa Tuzo za Kili Musc Award 2012 katika onesho lao la Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya jana.
Roma akipanda juukwaani akisindikizwa na DJ maarufu DJ Choka, alishangiliwa vilivyo na umati wa watu uliofurika uwanjani hapo pale tu ilipofika zamu yake kupanda jukwaani.
Roma! Roma! Roma! Roma!....hayo ndio yalikuwa maneno ya shwangwe kutoka kwa wapenzi wa burudani kutoka Jijini Mbeya waliofurika katika Uwanja wa Sokonine mjini hapa kushuhudia show hiyo kali ya Washindi wa Tuzo za Kili Music Award 2012.
Roma baada ya kumaliza kuimba nyimbo zake kaza aliwashukuru wana Mbeya kwa kura zao zilizompa ushindi na kuwaambia sasa anamaliza show hiyo ambayo hadi hapo alipofikia alisema wametumia Sh 200/= pekee kati ya Sh 2,000 ya kiingilia waliyotoa.
“Sasa ndugu zangu, nawaambia ukweli hadi sasa mmesha tumia sh 200 tu ya kiingilio chezu,..sasa nawapa show ya Sh 1,800 iliyobaki,” alijigamba Roma ambaye muda wote alikuwa akishangilia na ndipo alipomaliza kwa kuimba Wimbo wa Mathematic uliompa tuzo.
Wasanii wengine waliopanda jukwaani hii leo ni pamoja na Ben Pol, AT, Ali Kiba , Barnaba, Omy Dimpoz  na Suma Lee nao wamefunika vibaya katika Tamasha la Kili Music Award Winners Tour lililofanyika katika Uwanja wa sokoine Mjini Mbeya.
Alianza jukwaani kupanda mshindi wa Tuzo ya wimbo Bora wa R&B.
Msanii Ben Paul ambaye alijinyakulia tuzo hiyo kupitia kibao Number One ambapo nae alishambulia jukwaa na kuwaamsha watu kuwa sasa show imeanza.
Alifuata jukwaani Suma Lee ambaye aliongozwa na show kali kutoka kwa vijana wake wane wakike na wakiume na kushangiliwa vilivyo kwa mkongwe huyo wa Bongo Fleva.
Baada ya Ben Pol, alipanda mkali kutoka Zanzibar ambaye ni mshindi wa Tuzo Wimbo Bora wenye Vionjo vya Kiasili AT na kutoa burudani ya nguvu na  wimbo wa  Vifuu Utundu amabao ulimpa tuzo aliucheza vilivyo na wanenguaji wake wawili wa kike.
Ika fika zamu ya Omy Dimpoz jukwaani kwa kuimba nyimbo yake mpya aambayo alitaraji kuizindua jana katika Ukumbi wa Club Bilicanas jijini Dar es Salaam, single ya Baadae kasha  ile iliyo mpa tuzo ya Wimbo bora wa Kushirikishwa ya Nai Nai aliyo anza kuimba pekeyake na baade kuurudia wimbo huo akiwa na Ali Kiba.
Ali Kiba alibaki jukwaani hapo kama ilivyokuwa mjini Moshi na vijana wake kumfuata kutoa shukrani zao za kupata kura zilizo wapa ushindi wa tuzo ya Wimbo bora wa Zouk Rhumba kupitia wimbo wa Dushelele.
Wakati mara zote pazia la utoaji burudani kwa washindi hao wa tuzo za Kili Music Award 2012 wanaofanya ziara limekuwa likifunga na Roma Mkatoliki leo akapnda wapili kutoka mwisho.
Roma ambaye ni Mshindi wa tuzo mbili za Wimbo Bora wa Hip Hop kupitia wimbo wake wa Mathematics na Tuzo ya Msanii bora wa Hip Hop, alishambulia jukwaa huku viitikio vyake vikiimbwa na DJ Choka na hata alipomaliza show yake bado mashabiki walimtaka aendelee.
Mshindi wa Tuzo ya Mwimbaji bora wa Kiume, Barnaba ndiye aliyefunga pazia hilo kwa siku ya leo mjini Mbeya kwa kuimba  ikiwapo inayovuma kwa sasa ya Magube Gube.
Wasanii hao wiki ijayo wanataraji kutoa burudani kama hiyo jijini Mjini Mtwara na tayari walisha tumbuiza na kuwashukuru mashabiki wao wa Mkoani Dodoma na Jijini Mwanza na Moshi

MALAWI KUMCHAGUA FIRST ELEVEN POULSEN STARS

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Kim Poulsen (pichani kushoto) amesema atautumia mchezo wa kirafiki wa Kimataifa kati ya timu yake na Malawi uliopangwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi ijayo kupata kikosi cha kwanza cha timu hiyo. 
Gazeti la serikali, Habari Leo la leo limeandika; Kim kama ambavyo anapenda kuitwa ili kumtofautisha na kocha aliyemtangulia Jan Poulsen alisema hayo baada ya mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jana asubuhi kuwa atautathmini uwezo wa wachezaji wa timu hiyo kwenye mechi na kupata kikosi kitakachoivaa timu ya Taifa ya Ivory Coast Juni 2 Abijan. 
Taifa Stars imeweka kambi yake kwenye Hoteli ya Tansoma iliyopo Kariakoo jijini Dar es 
Salaam ikijiandaa na mchezo wa awali wa kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Brazil 2014 dhidi ya Ivory Coast ambayo ni miongoni mwa miamba ya soka ya Afrika lakini Kim haonekani kuingiwa hofu na mechi hiyo. 
“Ndio nafahamu Ivory Coast ni timu kubwa inayoundwa na wachezaji wazoefu, hiyo ni changamoto kwangu na nafurahia kucheza na timu za namna hiyo,”alisema Kim. 
Akizungumzia falsafa yake ya ufundishaji Kim tofauti na makocha wengi wanaopenda mfumo 
wa soka la kujihami hasa wanapoanzia ugenini alisema falsafa yake ni kucheza soka la kushambulia na kuhakikisha washambuliaji wa timu wanatumia vyema kila nafasi watakayoipata. 
“Nitashambulia nikiwa Abijan na nitataka wachezaji wangu kutumia kila nafasi itakayopatikana kwenye mchezo huo, lakini pia lazima tujilinde vizuri ili tusifungwe,” alisema Kim. 
Ingawa alisema kuwa kwa sasa anauwazia mchezo wa kirafiki dhidi ya Malawi Jumamosi ijayo kwani ndio utakaompa picha ni kwa kiwango gani wachezaji wa timu hiyo wamepokea 
mafundisho yake. 
Alisifu ushirikiano unaoneshwa na wachezaji wazoefu wa timu hiyo kuwasaidia wachezaji 
chipukizi katika kushika na kuelewa mafundisho yake. 
Wachezaji wote wamejiunga na kambi ya timu hiyo isipokuwa washambuliaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, ambao alisema wanamalizia mechi ya mwisho ya Ligi Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na watawasili nchini kesho kuungana na wenzao. 
Mbali na washambuliaji hao pia alikosekana kiungo mchezeshaji wa Simba Haruna Moshi 
ambaye yuko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo alikosindikiza msiba wa kiungo wa Simba 
Patrick Mafisango aliyefariki kwa ajali ya gari Alhamisi.

MAFISANGO ANAZIKWA LEO

MWILI wa kiungo wa Simba, Patrick Mutesa Mafisango unatarajiwa kuzikwa leo nyumbani kwao Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 
Gazeti la serikali, Habari Leo la leo, limeandika kwamba Mafisango aliyefikwa na mauti usiku wa kuamkia Alhamis baada ya kupata ajali ya gari, mwili wake ulisafirishwa alfajiri jana kuelekea Kinshasa na kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga msafara huo ulifika salama. 
Mwili wa mchezaji huyo kipenzi cha Wanasimba uliagwa juzi kwenye Uwanja wa TCC 
Chang’ombe kabla ya safari ya uwanja wa ndege tayari kwenda kwenye makazi yake ya milele. 
Nalo Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limetuma salamu za 
rambirambi kwa uongozi wa Simba, Watanzania na wapenda soka wote wa ukanda wa Afrika 
Mashariki na Kati. 
Katika taarifa yake jana, Katibu wa Cecafa, Nicholaus Musonye alisema Baraza lake limeshtushwa na taarifa za msiba wa Mafisango kwani ameondoka akiwa kijana mdogo. 
“Bado wanasoka walikuwa wakiuhitaji mchango wake, alikuwa mchezaji mahiri sana 
aliyejizolea umaarufu katika ukanda wetu huu, tulikuwa naye kwenye mashindano ya Kombe la Kagame, Kombe la Chalenji, lakini tumuombee tu afike salama,” alisema. 

Comments