CHAMA cha Makocha wa Riadha Tanzania (CHAWARITA),
kimelipongeza Baraza la Michezo la Taifa (BMT), chini ya Mwenyekiti wake,
Dioniz Malinzi kwa kufanikisha uchaguzi mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT),
uliofanyika mjini Morogoro Jumapili iliyopita na kupatika viongozi wapya chini
ya Rais Anthony Mtaka.
Akizungumza mjini hapa, Katibu Mkuu wa CHAWARITA,
Mwanariadha mahiri wa zamani, Nobert Kilimtali, alisema, wanampongeza Malinzi
na Baraza kwa ujumla, kwa kuhakikisha mikoa yote Tanzania
inafahamu kuna Riadha Tanzania
na kuwaita Morogoro kushiriki katika uchaguzi huo.
Kilimtali alisema, pia wanawapongeza waliochaguliwa, ila
watambue wamepewa madaraka na kuna kazi kubwa kuhakikisha wanaibua vipaji vya
nyota wa zamani kama akina Filbert Bayi, Juma Ikangaa, Gidamis Shahanga,
Zakaria Barrie, Gidamis Shahanga, Alfredo Shahanga, Mwinga Mwanjala, Rehema
Killo, Zebedayo Bayo, John Yuda, Lwiza John na wengineo wengi.
“Pia uongozi mpya upokee changamoto ya kuhakikisha mchezo wa
riadha unaanzia chini shuleni na unachezwa mikoa yote, tofauati na ilivyo hivi
sasa,” alisema.
Katibu huyo, aliwapongeza wagombea waliothubutu ingawa kula
zao hazikutosha, sambambna na viongozi waliokuwa madarakani na kukubali
uchaguzi ufanyike na kuwataka wasisite kushirikiana na uongozi mpya.
Uongozi mpya wa RT uliongia madarakani Jumapili ya Mei 22
katika uchaguzi uliofanyika hoteli ya Hilux mjini Morogoro ni pamoja na Rais
Anthony Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya (DC), ya Mvomero mkoani Morogoro,
Makamu wa Rais Utawala, William Kallaghe, Makamu wa Rais Ufundi, Dk. Ahmed
Ndee, Katibu Mkuu, Mujaya Suleiman Nyambui, Katibu Msaidizi, Ombeni Zavalla,
Mweka Hazina, Is-Haq Suleiman, huku wajumbe wa Kamati ya Utendaji ni Mwinga
Mwanjala, Meta Petro, Peter Mwita, Tullo Chambo, Rehema Killo, Lwiza John,
Zakaria Barrie, Zakaria Gwanda, Robert Kalyahe na Christian Matembo.
Comments
Post a Comment