KOCHA STARS AWAASA NYOTA WAKE KUTOWAHOFIA KINA DROGBAA DROGBA


KOCHA mkuu wa timu ya Taifa Taifa Stars amewataka wachezaji wake kutohofia nyota waliopo katika kikosi cha  Ivory Coast  kwani hawana tofouti na wao.
Stars na Ivory Coast watkawaana  Juni 2, mjini Abidjan, katika mechi ya kuwania kucheza fainali za kombe la
dunia ambapo kikosi cha Ivory Coast kinawachezaji wanaosakata soka la kulipwa barani Ulaya wakiwemo  Didier Drogba, . Yaya Toure na Solomon Kalou na wengineo.
Kim alisema wanaiheshimu Ivory Coast kama moja ya timu yenye wachezaji wazuri lakini hawaihofii kwani wachezaji wa Stars pia ni wazuri ingawa wanatofaitiana vitu vidogo vidogo tu.
Kocha huyo aliwataka wachezaji wake kupambana kadiri wawezavyo katika mchezo huo kwani  ndio siri ya ushindi na mafanikio ya timu yoyote.

Comments