BOBAN AENDELEZA VITUKO KUELEKEA SUDAN

KIUNGO mshambuliaji wa timu ya Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ jana alikuwa kivutio kwa mashabiki, wasindikizaji na hata baadhi ya wasafiri waliomuona wakati wakiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, kuelekea Sudan. Simba inakwenda Sudan katika mchezo wa marudiano dhidi ya Al Ahli Shendi utakaopigwa Jumapili, huku ikiwa na mtaji wa ushindi wa mabao 3-0, iliyoupata kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Uvaaji wa Boban, ndio uliowavutia watu kumtizama, kutokana na kuvaa kama mtu asiyesafiri. Boban alikuwa amevaa fulana, suruali ya kimichezo ‘trakisuti’ na kandambili, hivyo kusababisha watu kuvutika kumuangalia, huku baadhi yao wakibaki kujiuliza kuhusu vituko vya nyota huyo ambaye mashabiki humuita Balotteli wa Bongo. Mchezaji huyo anafananishwa na mshambuliaji mahiri wa Italia, anayekipiga klabu ya Manchester City ya England, ambako mara kwa mara amekuwa akibeba vichwa vya habari katika magazeti ya England na Ulaya kutokana na vituko vyake. Ukiondoa vituko hivyo vya uvaaji wa Boban, msafara wa watu 25 wakiwamo viongozi watano na wachezaji 20 wa timu hiyo waliondoka chini ya uongozi wa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Hussein Mwamba, majira ya saa 8:00 mchana

Comments

  1. Utajulikanaje bwana...tupo pamoja ndugu yangu!

    ReplyDelete

Post a Comment