AMOS MAKALLA AJITOA SIMBA SC

Mh.Makalla akitunuku nahodha wa Simba Juma Kaseja wakati wa sherehe za ubingwa wa Simba zilizofanyika Dar Live jumapili.


NAIBU Waziri wa habari, Vijana , Utamaduni na Michezo Amos  Makalla amejitoa kattika kamati ya fedha ya klabu ya soka ya Simba.
Makalla  aliteuliwa na kamati ya utendaji ya Simba chini ya mwenyekiti wake Simba Ismail Aden Rage mwezi oktoba mwaka jana  sambamba na Geofrey Nyange 'Kaburu' ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo na makamu wake ni Adam Mgoyi, wajume wengine ni pamoja na  Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe, katibu mkuu wa zamani wa Simba, Kassim Dewji na mdhamini wa zamani wa klabu hiyo Azim Dewji ni pamoja na Said Pamba,Juma Pinto, Abdul Mteketa na Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu.
Hata hivyo, Makala ambaye ni mbunge wa Mvomero alitangaza kujitoa nafasi hiyo kutokana na nafasi ya Unaibu Waziri na kusema kuwa analazimika kufanya hivyo ili kuweza kuvisaidia vilabu vya michezo yote nchini.

Comments

Post a Comment