WARENO WAMJERUHI MBAVU JT

Terry kushoto na Di Matteo

KOCHA wa Chelsea, Roberto Di Matteo amesema kwamba John Terry aliumia mbavu katika mchezo wa jana The Bluesm ikishinda 2-1 dhidi ya Benfica na kutinga Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Terry alitolewa baada ya saa moja kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, lakini Di Matteo anatumai tatizo hilo halitakuwa la muda mrefu.
Tatizo hilo linaweza kuisha Alhamisina akawahi mechi ya Chelsea na Wigan Athletic Jumamosi.
Chelsea sasa itakutana na Barcelona, ambayo inatazamiwa kutetea ubingwa wake.
The Blues wataingia kwenye mechi hiyo kama underdogs, lakini Di Matteo amesema kwamba watajitahidi kucheza kwa uwezo na mipango yao kupambana na wakali wa Barca akiwemo mwanasoka bora wa dunia, Lionel Messi.
"Itakuwa babu kubwa kucheza mechi mbili na moja kati ya timu bora duniani,' alisema Di Matteo.

Comments