WAREMBI MISS UKONGA, TABATA WAFANYA MAZOEZI YA PAMOJA

 Warembo wa kitongoji cha Ukonga wenye tisheti za orange na wale wa Tabata wenye tisheti za blue katika pozi mara baada ya ya Miss Tabata kutembelea kambi ya MIss Ukonga
 Miss Ukonga wakionyesha utaalamu wao
 Mmoja ya warembo wa Miss Tabata akipita jukwaani



Waratibu wa TAbata na Ukonga wakibadilishana MAwazo.


WAREMBO wa vitongoji viwili vya Ukonga na Tabata jana walifanya mazoezi ya pamoja katika kuleta ushirikiano na kujenga urafiki baina ya warembo hao katika fani ya urembo.
Warembo wa Tabata waliwatembelea wenzao wa Ukonga katika kambi yao ya mazoezi iliyopo Ukonga Hill Tech Bar maeneo ya Minazi Mirefu au maarufu Banana.
Vitongoji vya Ukonga na Tabata warembo wake watakao shinda wanataraji kukutana katika Kambi ya kanda ya Ilala kabla ya kwenda kushiriki shindano la taifa la Miss Tanzania 2012.
Wakizungumza jana baadhi ya warembo wa Ukonga wamesema ushirikiano wao huo na wenzao wa Tabata unawapa uwezo wa kijiamini na kupata nafasi ya kujifunza kile ambacho wenzao wanakifanya au wamejifunza ikiwa ni pamoja na utembeaji, uongeaji wa kati wa kujitambulisha na vitu vingine vingi.

“Tunawashukuiru sana waandaji wetu, maana mbali ya kuwa tunapata wageni wa aina mbalimbali ambao ni wadau wa urembo lakini leo tupo na washiriki wenzetu wa tabata ambao tunaimani tutakutana katika shindano la Ilala”, alisema Amina Sangawe.
Nae Suzanne Deodatus ambaye ni Mshiriki kutoka Tabata alisema wamepata fursa ya kujifunza mambo kabdhaa na wamefurahi sana kuwatembelea warembo wa Ukonga na kufnya nao mazoezi ya pamoja.
Mapema Mwezi huu warembo wa Ukonga waliwasindikiza Miss Tabata 2012 katika show yao kubwa ya Utambulisho iliyofanyika katika Ukumbi wa Dar West Tabata.
Shindano la Miss Ukonga 2012 linataraji kufanyika Mei 5, mwaka huu na lile la Tabata linataraji kufanyika mapema mwezi Juni.

Comments