WAARABU KUCHEZESHA SIMBA V ES SETIF KESHO


Wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), Simba kesho (Aprili 6 mwaka huu) wanapambana na ES Setif katika mchezo wa marudiano wa kombe hilo. 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunaitakiwa kila la kheri Simba kwenye mechi hiyo kwani ina uwezo wa kupata matokeo mazuri yatakayoivusha katika raundi inayofuata. Msafara wa Simba unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Dk. Sylvester Faya. 
Mechi hiyo namba 46 itachezeshwa na waamuzi Ben Hassan Mohamed, Hmila Anouar, Ben Abdelmoumen Kamel na Kordi Med Said, wote kutoka Tunisia. Kamishna atakuwa Jean Fidele Diramba kutoka Gabon.
 

Comments