TSUNAMI YAZUIA KAMBI YA SIMBA

KUWEPO kwa tishio la Tsunami jana jioni kumepelekea klabu ya soka ya Simba kubadili mpango wao wa kuingia kambini kujiandaa na mechi zao za Ligi Kuu soka Tanzania Bara.
Simba ambayo inatarajiwa kukwaana na Ruvu Shooting jumapili hii kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mchezo wa ligi hiyo ilitarajiwa kuingia kambini kwenye hoteli ya Bamba Beach Kigamboni jana jioni.
Ofisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga alisema baada ya kupata taarifa za mabadiliko ya hali ya hewa imebi kutulia kwanza na ndipo watajua mustakabali mzima wa maandalizi ya timu hiyo ambayo inaiwakilisha Tanzania kwenye kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF) ikiwa imetinga hatua ya 16 bora ambapo inatarajiwa kukwaana na Al Ahly Shandy Aprili 22 jijini Dar es Salaam.

Comments