TIBAIGANA KUAMUA MBIVU NA MBICHI YANGA KESHO


Kikao cha Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kilichokuwa kifanyike kesho (Aprili 14 mwaka huu) kujadili rufani ya Yanga kupinga kunyang’anywa pointi tatu kwa kumchezesha Nadir Haroub katika mechi dhidi ya Coastal Union kimeahirishwa. 
Kamati hiyo chini ya uenyekiti wa Kamishna mstaafu wa Polisi, Alfred Tibaigana sasa kitafanyika Jumanne (Aprili 17 mwaka huu) saa 9 alasiri kwenye ofisi za TFF.

MIKOA 13 YAWASILISHA MABINGWA WAKE
Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa 17 ya Tanzania Bara vimewasilisha majina ya mabingwa wake kwa ajili ya Ligi ya Taifa iliyopangwa kuanza Aprili 22 mwaka huu katika vituo vitatu. 
Mikoa hiyo na mabingwa wake katika mabano ni Kigoma (Kanembwa FC ya Kibondo), Kilimanjaro (Forest FC ya Siha), Ruvuma (Mighty Elephant ya Songea), Dodoma (CDA), Rukwa, (Mpanda Star ya Mpanda), Iringa (Kurugenzi FC ya Mufindi) na Lindi (Lindi SC). 
Mingine ni Mtwara (Ndanda FC), Shinyanga (Mwadui FC), Mara (Polisi Mara), Singida (Aston Villa), Arusha (Flamingo SC) na Tabora (Majimaji FC). Mikoa ambayo haijawasilisha mabingwa wake ni Manyara, Dar es Salaam, Mwanza, Tanga, Morogoro, Pwani na Kagera. 
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Comments