TBL WADHAMINI WAPYA TAIFA STARS


Taifa Stars ilipokuwa ziarani Denmark enzi za udhamini wa SBL
BIA ya Kilimanjaro Premeum Lager rasmi ndio mdhamini mpya wa timu ya taifa ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, bongostaz imeipata hiyo.
Bia hiyo inayozalishwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wiki hii itafanya hafa maalum ya kuutangaza rasmi udhamini huo.
Chanzo cha habari kutoka TBL, kimesema hafla hiyo itafanyikia katika hoteli ya Serena, iliyokuwa Royal Palm Movenpick, Dar es Salaam wiki hii.  
Tangu mwaka 2006, Taifa Stars imekuwa ikidhaminiwa na Serengeti Breweries Limited ambao wameshindwa kuingia mkataba mpya na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kwa sababu ya kupandishiwa dau. 
Baada ya mkataba wao (SBL) kufikia tamati Desemba, mwaka jana, TFF ikaipandishia dau la udhamini kutoka Sh. Bilioni 1.2 hadi Bilioni 3.6, ambayo ni zaidi ya asilimia 300.
TBL imekubali kuidhamini Stars kwa dau la Sh. Bilioni 3.6 kwa mwaka.

Comments