SIMBA WAJICHIMBIA KIDONGO CHEKUNDU

WEKUNDU wa Msimbazi, Simba wameingia kambini jioni ya leo kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wao wa kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Shandy ya Sudan utakaopigwa jumapili hii kwenye dimba la Taifa jijini Dar es Salaam.
Taarifa ambazo mamapipiro blog imezinasa zinaeleza kuwa kikosi cha Simba kimeingia kambini katika hoteli moja iliyopo eneo la Kidongo Chekundu mara baada ya kumaliza mazoezi yake ya jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Comments