SIMBA TAYARI WAPO CAIRO


Mafisango na Machaku Uwanja wa Ndege Cairo

WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya Afrika, Simba SC tayari wapo mjini Cairo, Misri wakiwa njiani kuelekea Algeria.
Simba waliondoka alfajiri ya leo Dar es Salaam kuelekea Algeria kwa ajili ya mechi ya marudiano, Raundi ya Pili Kombe la Shirikisho la Soka Afrika dhidi ya wenyeji ES Setif, wakipitia Algeria.
Simba walioondoka wakiwa na matumaini makubwa ya kuitoa ES Setif katika mchezo huo utakaofanyika Ijumaa wiki hii, ina mpango wa kukaa kwa siku mbili Cairo kabla ya kuunganisha kwenda Algeria.
Viongozi waliofuatana na timu ni Mwenyekiti wa Ismail Aden Rage, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo Damian Manembe na Ofisa Habari, Ezekiel Kamwaga.
Wengine ni Kocha Mkuu, Milovan Cirkovic, Kocha Msaidizi Amatre Richard, kocha wa makipa James Kisaka, daktari wa timu Cosmas Kapinga, Meneja Nico Nyagawa na mtunza vifaa Kessy Rajab.
Wachezaji waliopo kwenye msafara ni Juma Kaseja, Ally Mustafa, Nassor Masoud, Shomari Kapombe, Amir Maftaha, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, Victor Costa, Obadia Mungusa, Jonas Mkude, Patrick Mafisango, Mwinyi Kazimoto, Haruna Moshi, Salum Machaku, Uhuru Suleiman, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Edward Christopher, Derick Walulya na Gervais Kago.
Simba ilishinda mchezo wa kwanza wiki moja iliyopita mabao 2-0, hivyo sare ya aina yoyote au isipofungwa zaidi ya bao 1-0 itakuwa imesonga mbele.
Katika mchezo huo, Simba baada ya ushindi wa awali wa 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, inahitaji hata sare au kufungwa si zaidi ya 1-0 ili kusonga mbele.  

Comments