SIMBA, SHOOTING ZAINGIZA MIL 40/-

Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Ruvu Shooting na Simba lililochezwa juzi (Aprili 15 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 40,855,000.
Jumla ya watazamaji 10,824 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa viingilio vya sh. 3,000, sh. 5,000, sh. 10,000 na sh. 15,000. Watazamaji 8,500 kati ya hao walishuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 3,000.
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 6,232,118.64 kila klabu ilipata sh. 7,406,424.41, uwanja sh. 2,468,808.14.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 2,468,808.14, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 493,761.63 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) sh. 493,761.63.
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,234,404.07, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 246,880.81 na asilimia 10 ya gharama za mechi ni sh. 2,468,808.14.
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000 na nauli ya ndani kwa mtathmini wa waamuzi sh. 10,000.
Mwamuzi wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna, mtathmini wa waamuzi na waamuzi sh. 200,000, gharama ya tiketi sh. 2,460,000, maandalizi ya uwanja (pitch) sh. 400,000, umeme sh. 300,000, usafi na ulinzi kwa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000.
Gharama nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi; kila klabu ilipata sh. 757,680 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) kilipata sh. 649,440.
Nayo mechi kati ya Villa Squad na Coastal Union iliyochezwa Aprili 15 mwaka huu kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam iliingiza sh. 499,000 ambapo kila klabu ilipata sh. 44,374 wakati watazamaji walioshuhudia mechi hiyo ni 451.
Vilevile mechi kati ya Moro United na JKT Oljoro iliyochezwa Aprili 14 mwaka huu Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam iliingiza sh. 410,000 kutokana na washabiki 402. Kila klabu ilipata sh. 39,257.


7,186 WASHUHUDIA MECHI YA TOTO AFRICANS, YANGA
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Toto Africans na Yanga iliyochezwa juzi (Aprili 15 mwaka huu) kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ilishuhudiwa na watazamaji 7,186 na kuingiza sh. 15,392,000. Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000 kwa jukwaa kuu na sh. 2,000 mzunguko. 
Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 2,347,932 kila klabu ilipata sh. 2,729,060, uwanja sh. 909,686. 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 909,686, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) sh. 363,874, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 454,843, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 90,968 na asilimia 10 ya gharama za mechi ni sh. 909,686. 
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000. Mwamuzi wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa kamishna na waamuzi sh. 160,000, gharama ya tiketi sh. 2,300,000. 
Gharama nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila tiketi; kila klabu ilipata sh. 503,020 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) kilipata sh. 431,160.

Comments