RAIS ZFA AJIVUA GAMBA

RAIS wa chama cha soka visiwani Zanzibar (ZFA) Ali Ferej Tamim amejiuzulu.
Habari kutoka visiwani Zanzibar zinasema kwamba Tamim aliyekaa madarakani kwa miaka 20 amewasilisha barua ya kujiuzulu kwake kwa kaimu Katibu Mkuu wa ZFA, Masoud Attai.
Tamim ameamu kujitoa katika nafasi hiyo kwa madai ya suala la afya sambamba na kuangalia familia yake.
Alisema amechua uamuzi huo bila ya kushinikizwa na yoyote.
Kwa muda mrefu ZFA chini ya uongozi wa Tamim imekuwa ikilaumiwa kuchangia kuzorota kwa maendeleo ya soka visiwani humo, huku hali ikionekana kuchafuka hadi kwenye uchaguzi mkuu wa chama hicho mwaka juzi kutokana na kuwepo kampeni ya kutaka viongozi waliokuwa madarakani kutaka waendelee kuongoza.
Hata hivyo kamati ya uchaguzi ilitaka zoezi la uchaguzi lirudiwe mwaka jana ambapo baadhi ya wagombea walijitoa na mwisho wa siku waliorejea madarakani walikuwa walewale viongozi wa zamani.

Comments