MAN UNITED KUZIDI KUPAA ENGLAND LEO?


Ferguson kulia na Scholes
KOCHA Sir Alex Ferguson hana majeruhi wapya kikosi mwake kuelekea mechi ya leo na zaidi atakuwa na nguvu mpya ya kurejea kwa Nani, ambaye amekosa mechi tano zilizopita kwa maumivu ya kifundo cha mguu.
Bosi huyo wa United anatarajiwa kufanya mabadiliko kikosi mwake baada ya timu hiyo kwa sababu ya mechi tatu katika wiki moja.
Pamoja na hayo, anatarajiwa kumpanga winga aliye katika fomu ya juu, Antonio Valencia na  hiyo maana yake Ashley Young ataanzia benchi.
Michael Owen hajapona sawasawa kiasi cha kucheza leo Uwanja wa Old Trafford na pamoja na hayo, chaguo kuu la Sir Alex katika safu ya ushambuliaji itakuwa ana ni kuwapanga pamoja Wayne Rooney na Danny Welbeck au Javier Hernandez.
Mabadiliko mengine, Chris Smalling anaweza kuchukua nafasi ya Rafael na Paul Scholes akampisha Phil Jones.
Kocha wa QPR, Mark Hughes atamkosa Djibril Cisse anayetumikia adhabu, ambaye atakosa mechi ya pili katika adhabu yake ya kufungiwa mechi nne. Armand Traore na Fitz Hall bado hawatakuwapo.
Pamoja na hayo, wote DJ Campbell na Heidar Helguson wamerejea kikosini baada ya kuwa nje kwa muda.

JE WAJUA?
•Manchester United ikishinda leo inaweza kufikisha poini nane za kuwazidi wapinzani wao katika mbio za taji la Ligi Kuu, Manchester City, japo kwa saa kadhaa.
 •Mashetani Wekundu wameshinda mechi 10 katika mechi zao 11 zilizopita, ikishinda mechi saba mfululizo.
•Vijajna wa Sir Alex wamewafunga QPR mara tisa katika mechi 12 zilizopita baina yan timu hizo.
 •United imefungwa mechi mbili tu katika mechi zao 36 walizocheza kwenye Uwanja wa Old Trafford, wameshinda 32.
 •Vinara wa Ligi Kuu wamefungwa bao moja tu katika mechi tano zilizopita za ligi nyumbani.
 •Antonio Valencia ametoa pasi za mabao 12  na kufunga mabao manne katika mechi zake 16 alizocheza za ligi hadi sasa.
 •QPR imefungwa mechi 15 kati yas 19 zilizopita kwenye Uwanja wa at Old Trafford,ilishineda moja tu.
 •Vijana wa Hughes walibeba pointi mbili tu katika mechi 9 zilizopita.
 •Lakini wanaweza kutiwa nguvu na ushindi wao dhidi ya Arsenal wiki iliyopita wa 2-1 kwenye Uwanja wa Loftus Road..
 •Anton Ferdinand, kaka wa beki wa United, Rio, amejifunga katika mechi mbili zilizopita alizokwenda Old Trafford.
 •Rangers imeshindwa kulinda nyavu zake kuguswa katika mechi 12 nje ya Uwanja wa nyumbani.
PROBABLE LINEUPS
MANCHESTER UNITED: De Gea, Smalling, Ferdinand, Evans, Evra
Valencia, Jones, Carrick, Nani, Rooney na Welbeck.
QPR: Kenny, Young, Ferdinand, Onuoha, Taiwo, Mackie, Barton, Derry, Diakite, Taarabt na Zamora.

Comments