MAN CITY YAPIGA MTU SITA, TEVEZ PEKE YAKE TATU


Tevez
MUARGENTINA Carlos Tevez amepiga hat-trick akiisaidia Manchester City kuitandika Norwich 6-1 na kupunguza pengo la pointi wanazozidwa na Manchester United hadi mbili katika Ligi Kuu ya England.
United itacheza na Aston Villa kesho.
Tevez alifunga dakika ya 18, 73 na 80 wakati mabao mengine yalitupiwa na Aguero dakika ya 27 na 75 na Johnson dakika ya 90, wakati la wapinzani wao lilifungwa na Surman dakika ya 51.
Licha ya kocha wa City, Roberto Mancini kukata tamaa ya kuwakamata watoto wa Sir Alex Ferguson msimu huu, lakini ushindi huu bila shaka hata yeye unamfanya aone inawezekana. 

Comments