DARAJA LA KWANZA YAENDELEA LEO


LIGI Daraja la Kwanza Tanzania Bara, inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo kati ya Mgambo Shooting ya Tanga na Polisi Tabora Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Mgambo ndio inaoongoza ligi hiyo kwa pointi zake 11 wakati Polisi Tabora ina pointi nne. Mechi ya pili itakuwa kati ya Polisi Morogoro yenye pointi kumi na Polisi Dar es Salaam yenye pointi sita.
Mechi ya pili itakuwa kati ya Polisi Morogoro yenye pointi kumi na Polisi Dar es Salaam yenye pointi sita.
Jana Tanzania Prisons ya Mbeya na Mlale JKT ya Ruvuma zimetoka sare ya bao 1-1 katika mchezo wa fainali za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) uliochezwa leo (Aprili 14 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini hapa.
Kwa sare hiyo Tanzania Prisons imefikisha pointi nane wakati Mlale JKT inazo tano. Timu tatu za kwanza katika fainali hiyo ya 9 bora zitapanda kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao.
Mlale JKT ndiyo walioanza kufunga dakika ya 61 kwa mpira wa adhabu uliopigwa nje ya eneo la hatari na mshambuliaji Edward Malimi katika mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi Shabani Shata kutoka Kigoma.
Dakika sita kabla ya filimbi ya mwisho beki Richard Mwakalinga aliisawazishia Tanzania Prisons inayofundishwa na Stephen Matata baada ya kufanya shambulizi kubwa langoni mwa Mlale JKT.
Hadi tuna kwenda mitamboni, mechi ya pili kati ya Rhino Rangers ya Tabora na Mbeya City ya Mbeya ilikuwa ikiendelea huku Rhino Rangers ikiwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa dakika ya 18 na kiungo Salum Tabayi.

Comments