CHELSEA YAIBWAGA BARCA DARAJANI

Mshambuliaji wa Chelsea, Didier Drogba akishangilia bao lake pekee alilofunga dakika ya pili ya dakika za majeruhi baada ya kutimu dakika 45 za kipindi cha kwanza kwenye Uwanja wa Stamford Bridge, London, England usiku huu katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, dhidi ya mabingwa watetezi, Barcelona ya Hispania. Chelsea sasa inahitaji sare yoyote kwenye mchezo wa marudiano ugenini, Uwanja wa Camop Nou ili kutinga fainali, ambako itacheza na mshindi kati ya Bayern Munich ya Ujerumani na Real Madrid ya Hispania. Mechi ya kwanza jana mjini Munich, Real walifungwa 2-1 na wanahitaji ushindi japo wa 1-0 nyumbani, Santiago Bernabeu ili kutinga Fainali.

Comments