CHAMA CHA SOKA MTWARA CHAPATA VIONGOZI WAPYA

Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mtwara (MTWAREFA) kimepata viongozi wapya katika uchaguzi uliofanyika juzi (Aprili 15 mwaka huu) ukumbi wa Clinical Officers Training College wilayani Masasi.
Waliochaguliwa ni Athumani Kambi (Mwenyekiti), Vincent Majili (Katibu Mkuu), Kazito Mbano (Mhazini) na mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Fredrick Nachinuku.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa MTWAREFA walikuwa 30 ambapo Kambi alipata kura 23 za ndiyo na saba za hapana wakati Majili alipata kura 27 dhidi ya tatu za Charles Haule.
Nafasi nyingine hazikuwa na wagombea ambapo uchaguzi mdogo utaitishwa baadaye.

Comments