BREAKING NEWS: VIONGOZI WENGINE YANGA WAJIVUA GAMBA

HALI ndani ya klabu ya Yanga imeendelea kuwa tete baada ya viongozi wengine wawili muhimili ndamni ya klabu hiyo kutangaza kujiuzulu.
Habari ambazo mamapipiro blog imezinasa zimebaini viongozi hao ni pamoja na mumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga Seif Ahmed na mjumbe wa Kamati ya Ufundi, mashindano na usajili, Abdallah Binkleb.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Yanga zinaeleza kuwa viongozi hao wameamua kubwaga manyanga baada ya kuchposhwa na ubabaishaji unaofanywa na baadhi ya viongozi wa juu wa klabu hiyo na tayari wameshawasilisha barua kwa Mwenyekiti wa yanga, Lloyd Nchunga.

Comments