AFANDE SELE, 20% WASWEKWA RUMANDE




Na Ghisa Abby, Kilosa

WASANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini, Selemani Msindi, ‘Afande Sele’ na Abbas Kinzasa, ‘20%’ juzi walizua tafrani kubwa mjini Morogoro iliyowasababishia kutupwa rumande baada ya kukosa dhamana mahakamani.
Imeelezwa kuwa wasanii hao juzi, walifika na gari lao katika maeneo ya Benki ya NMB Tawi la Wami, ambako katika kupaki kulitokea kutoelewana na askari wanaolinda usalama, hivyo kuzuka kwa tafrani kubwa.
“Baada ya kutokea mzozo huo, wananchi nao wakaanza kuingilia, hivyo kuzuka tafrani kubwa, ikiwamo kuharibiwa kwa baadhi ya magari yaliyokuwapo eneo hilo na askari mmojawapo kuumizwa,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Ilibidi askari wafike na kutumia nguvu kuwatawanya wananchi, huku Afande Sele na 20% wakitiwa mbaroni na kufikishwa mahakamani jana, ambako walikosa dhamana na kutupwa rumande.”

Comments