MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara, Yanga ya jijini
Dar es Salaam, imejificha kwenye uwanja wa Shule ya Kimataifa ya Tanganyika
Masaki, kujiandaa na mechi yao
dhidi ya Coastal Union ya Tanga.
Mechi baina ya timu hizo, inatarajiwa kupigwa Machi 31, mwaka huu
kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga na Kocha wa Yanga, Kostadin Papic,
anauchukulia mchezo huo kama fainali.
Papic, ameamua kubadili uwanja wa mazoezi kutoka ule wa Shule ya Sekondari
Loyola uliopo Mabibo hadi huo wa Tanganyika bila ya kueleza sababu,
ingawa inadhaniwa ni kukwepa kutizamwa na mashabiki.
Msemaji
wa Yanga, Louis Sendeu, alisema kwamba wanashukuru hadi sasa hakuna majeruhi
mpya kwenye kikosi chao, zaidi ya kipa Yaw Berko anayeuguza goti.
Aliongeza kuwa wachezaji wanajifua kuhakikisha wanaibuka na ushindi
katika mchezo huo na mingine yote iliyobaki, ili kuhakikisha wanatetea ubingwa
wao.
Comments
Post a Comment