TIMU ya Villa Squad ya Magomeni Dar es Salaam, inayoburuza mkia katika
Ligi kuu ya soka Tanzania
bara imejitapa kuwa bado inayo matumaini ya kujinusuru na janga la kushuka
daraja.
Katibu Mkuu wa muda wa
Villa, Frank Mchaki, alisema kuwa wanaamini watakuwa kati ya timu zitakazobaki
na kucheza Ligi kuu mwakani licha ya kuwa mkiani.
Mchaki alisema wanaamini hivyo kutokana na molari walionao wachezaji
wao hivi sasa ambapo wanaamini watashinda mechi zao zote sita zilizosalia za
Ligi kuu.
Alisema kuwa tayari wameyafanyia masahihisho makosa yaliyojitokeza
katika mechi iliyopita dhidi ya Yanga ambayo walipoteza dakika ya mwisho ya
mchezo huo.
“Sisi Villa Squad tunapenda kuwaambia wana Kinondoni kuwa waendelee
kutuunga mkono tunawahakikishia kuwa tutabaki Ligi kuu, wasifikirie kabisa
suala la kushuka daraja,” alisema Machaki.
Alisema kwa pointi 16 walizonazo iwapo watashinda zote na timu zilizo
juu yake za Polisi Dodoma yenye pointi 17 na michezo minne mkononi, Moro Dodoma
yenye pointi 18 na michezo sita mkononi na African Lyon yenye pointi 18 na
michezo saba mkononi ndizo zitakazoshuka.
Aliongeza kuwa wachezaji wao wanaoendelea kujifua kwa nguvu zote
wameahidi kufia uwanjani kuhakikisha wanashinda mechi zote ili timu hiyo iweze
kubaki Ligi kuu msimu ujao.
Comments
Post a Comment