WAKATI
wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Shirikisho (CAF), Simba
ikitarajiwa kurejeana na Kiyovu ya Rwanda kwenye dimba la Taifa Jumapili,
kiingilo cha chini kimepangwa kuwa sh 5,000.
Kwa mujibu wa
taarifa zilizopatika jijini Dar es Salaam jana, kiingilio hicho kitahusisha
mashabiki watakaokaa viti vya rangi ya bluu na kijani, ili kutoa fursa kwa
mashabiki wengi kuhudhuria.
Taarifa hizo,
zinaeleza kuwa kiingilio cha juu katika mchezo huo ni sh 30,000, ambacho
kitahusisha mashabiki watakaokaa jukwaa la VIP A.
Aidha mashabiki
watakaokaa viti vya rangi ya chungwa watalipa sh 8,000, VIP C sh 20,000 na
VIP B watalipa sh 15,000 .
Comments
Post a Comment