Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kitengo cha
upelelezi wa miili ya marehemu ilisema kwamba kuzama kwa mwili wa mwanadada
huyo kulichangiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuzidiwa na dawa za kulevya na ugonjwa
wa moyo.
Taarifa hiyo iliendelea kupasha kuwa baada ya kufariki kwa Houston pembeni mwake
kulikuwa na dawa za kulevya aina ya Xanax, Flexeril, bangi na Benadryl ambazo
zimeonekana kuchangia kifo chake.
Taarifa hiyo inasema kwamba hakuna dawa aina ya cocaine
iliyopatika katika chumba alichokuwa amefia mwanadada huyo.
Msemaji wa upepelezi wa kitengo hicho, Craig Harvey,
alinukuliwa akisema kwamba kiasi cha cocaine kilionekana kwenye mfumo wake,
kikionyesha kwamba mwanadada huyo alikuwa amekubuhu katika matumizi ya dawa
hizo.
Comments
Post a Comment