SIKU moja baada ya Ofisa Habari wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura kutangaza kwa Mkoa wa Morogoro ndio uliopewa uenyeji wa fainali za Ligi daraja la Kwanza mwaka huu TFF imekanusha taarifa hiyo.
Kaimu Katibu Mkuu, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Sunday
Kayuni (pichani), amesema kuwa Chama cha Soka cha Mkoa wa Morogoro, (MRFA), hakijapewa
uenyeji bali kinayo nafasi kubwa ya kushinda uenyeji huo.
Kayuni alisema kuwa, usahihi
ni kwamba Morogoro ina nafasi kubwa kwa vile ndiyo pekee iliyotoa kiasi cha sh
mil 10,000 kati ya sh mil 25,000 ambazo zilikuwa moja ya masharti anayopaswa
kuyatekeleza mwombaji wa nafasi ya uenyeji wa fainali hizo.
Alisema kutokana na hilo Mkoa huo umepewa
hadi Machi 25 kumalizia kiasi cha fedha kilichosalia na iwapo itashindwa kamati
ya Ligi itakayoketi Machi 26 inaweza kutoa uamuzi wa kuinyang’anya nafasi hiyo.
“TFF tunapenda kusahihisha
taarifa iliyotolewa jana na Ofisa Habari kwamba Morogoro imepewa uenyeji wa
fainali za Ligi daraja la kwanza, usahihi ni kuwa Morogoro haijapewa nafasi
hiyo bali inayo nafasi kubwa ya kupewa uenyeji huo kwa sababu imelipa kiasi
kikubwa cha fedha, ambazo ni moja ya masharti ya kuomba uenyeji,” alisema
Kayuni.
Alisema kuwa Mikoa mingine
iliyoomba kupewa uenyeji huo licha ya kukumbushwa mara kwa mara lakini
haikuonyesha utayari kwani hakuna Mkoa uliolipa japo sehemu ya fedha hizo sh ml
25.
Timu zinazotarajiwa kushiriki
fainali hizo hiyo kutoka kundi A ni Polisi Dar es Salaam, Mgambo Shooting ya
Tanga na Transit Camp ya Dar es Salaam, Kundi B ni Mbeya City Council, Mlale
JKT ya Ruvuma na Tanzania Prisons ya Mbeya wakati C ni Polisi Tabora, Polisi
Morogoro na Rhino Rangers ya Tabora.
Comments
Post a Comment