SIR FERGUSON AWAPUUZA MAN CITY

Meneja wa klabu ya Manchester United Sir Alex Ferguson amepuuza kejeli kutoka kwa wakuu wa Manchester City juu ya uwamuzi wake wa kumsajili tena Paul Scholes aliyetangaza mwaka jana kustaafu mchezo wa soka.
Mcheza kiungo wa zamani wa klabu ya City na Arsenal, Patrick Vieira aliliambia gazeti moja katika mahojiano kua "ni dalili ya udhaifu".
Lakini Ferguson amewaonya kua ana silaha za kutosha ikiwa mahasimu wake wanataka kuanzisha vita vya maneno.
Aliongezea kusema kua ikiwa ni hali ya kutapatapa kumrejesha uwanjani mmojapo wa wacheza kiungo bora nchini Uingereza kwa kipindi cha miaka 20 basi nitakubaliana na dhana yao.
Viera, ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa maendeleo ya soka katika klabu ya City, aliliambia gazeti la Daily Telegraph siku ya jumatano kua: Kwake yeye Scholes kurudi uwanjani ni ishara ya udhaifu na kutapatapa kwa United kumrejesha mchezaji mwenye umri mkubwa wa miaka 37.
United imeshinda mechi tisa za Ligi kuu wakati Scholes anashiriki na kutoa sare ya mechi moja. Na kufuatia matamshi hayo, Ferguson akamjibu Mancini wiki ambapo alimruhusu mchezaji aliyezusha kasheshe Carlos Tevez.
"Roberto alituandama sisi. Ikiwa ni hivyo nasi tutaucheza mchezo huo huo. Silaha zipo tele.
Ferguson alisema "unaposema tunapatapa, wao wamemtumia mchezaji aliyekataa kushiriki mechi. Wakati huo Meneja aliapa kua hatomtumia mchezaji huyo abadan' na aliondoka na kwenda zake likizoni huko Argentina bila ruhusa ya klabu. Nieleze hayo, Je hilo tutasema ni kutapatapa?
Carlos Tevez alishiriki mechi ya jumatano Manchester City ilipoibwaga Chelsea 2-1 kuiweka pointi moja nyuma ya United zikisalia mechi tisa kuhitimisha Ligi ya Premier ya msimu wa mwaka 2011/2012.
CHANZO:BBC SWAHILI

Comments