SERENGETI BOYS WAINGIA KAMBINI

Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) leo (Machi 2 mwaka huu) imeanza kambi yake ya wiki moja ambayo hufanyika kila mwezi jijini Dar es Salaam chini ya kocha Kim Poulsen.
Serengeti Boys inayofanya mazoezi Uwanja wa Karume itahitimisha kambi hiyo Machi 9 mwaka huu kwa kucheza mechi na timu ya U20 ya Ruvu Shooting ya mkoani Pwani ambayo iko Ligi Kuu ya Vodacom.
Baada ya Serengeti Boys kumaliza kambi Machi 9 mwaka huu, siku hiyo hiyo timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) nayo itaingia kambini chini ya Poulsen katika mpango wa timu hizo kufanya mazoezi ya wiki moja kila mwezi na kucheza mechi moja.

Comments