RAUL AWAKABIDHI WAJERUMANI BAO LA 400


MSHAMBULIAJI wa Schalke 04, Raul amechangia jezi yake na bao lake la 400 alilofunga katika kumbukumbu ya soka ya Ujerumani.
Mpachika mabao huyo wa zamani wa kimataifa wa Hispania, Raul alifunga bao hilo Februari 19 katika ushindi wa 4-0 kwenye Bundesliga dhidi ya Wolfsburg.
"Nimekuwa na wakati mzuri sana Bundesliga na ninajivunia sana heshima niliyopewa na mashabiki wa Ujerumani," alisema Raul, ambaye amefunga mabao 33 tangu ajiunge na Schalke majira ya joto 2010.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34, amefunga mabao 323 akiwa na Real Madrid, ambako alianzia soka ya kulipwa mwaka 1994, na alitwaa mataji matatu ya Ligi ya Mabingwa.
Alifunga mengine 44 akiwa na timu ya taifa ya Hispania na 33 akiwa na Gelsenkirchen.

Comments