MMOJA ya washindi
wa shindano la muziki la Tusker All Stars 2011, Mtanzania Peter
Msechu amesema licha ya kazi zake kupokelewa vema na mashabiki,
hana mpango wa kutoa albamu.
Msechu ambaye kwa sasa anatamba na singo yake ya Relax aliyomshirikisha Kidum amesema kuwa amefikia uamuzi huo kutokana na unyonyaji
wa kazi za wasanii unaofanywa na baadhi ya wafanyabiashara.
Alisema wasanii wengi
wamekuwa wakitumia gharama kubwa katika kutayarisha albamu zao lakini mwisho wa
siku zinapoingia sokoni wanajikuta wakipata hasara huku wafanyabiashara hao
wakifaidika.
Comments
Post a Comment