LEO
Barcelona inaweza kupunguza pengo la pointi inazozidiwa na Real Madrid katika La
Liga na kubaki pointi tano, iwapo watashinda mechi dhidi ya wageni wao, Granada.
Hiyo
inafuatia Real kulazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Malaga juzi.
Kikosi
cha Jose Mourinho kilinyimwa ushindi wa 12 mfululizo kwa bao la dakika ya
mwisho la Santi Cazorla, hivyo kufufua matumaini ya Barca kutwaa taji la nne
mfululizo la La Liga.
Real,
ikiwa na pointi 71 dhidi ya 63 za Barca, zikiwa zimebaki mechi 11, wanakabiliwa
na mechi ngumu ugenini kesho dhidi ya Villarreal, ambao wanapigana kurejea
matawi ya juu.
Utakuwa
ni mtihani mgumu kwa Miguel Angel Lotina, kocha wa tatu Villarreal msimu huu, aliyetambulishwa
jana baada ya kufukuzwa kwa Jose Molina.
"Kwangu
inaonekana sare ni sehemu ya mchezo," alisema Mourinho baada ya mechi na Malaga.
"Sote
tunafahamu kuna mechi 11 zimebaki na pointi 33 mbele, ambayo inamaanisha mbio
za ubingwa bado zipo wazi," alisema Mreno huyo.
Comments
Post a Comment