Katibu wa Chama cha Waamuzi wa soka Tanzania (FRAT) Leslie Liunda akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na adhabu waliyopewa wachezaji wa Yanga baada ya kumpiga mwamuzi Israel Nkongo.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
20/03/2012
VURUGU ZILIZOTOKEA KWENYE MCHEZO WA VODACOM PREMIER LEAGUE
TAREHE 10/03/2012 KATI YA TIMU YA YANGA NA AZAM
ITAKUMBUKWA YA KWAMBA KWENYE MCHEZO KATI YA TIMU YA YANGA NA
AZAM MCHEZO WA VODACOM PREMIER LEAGUE TAREHE 10/03/2012 MWAMUZI WA MCHEZO HUO
ISRAEL NKONGO ALIPIGWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA TIMU YA YANGA KATIKA VURUGU
ZILIZOTOKEA DAKIKA YA KUMI NA MOJA YAMCHEZO, BAADA YA MWAMUZI HUYO KUFANYA
MAAMUZI SAHIHI YA KUMUONYESHA KADI YA PILI YA MANJANO NA KUFUATIWA NA KADI
NYEKUNDU MCHEZAJI WA YANGA HARUNA NIYONZIMA.
BAADA YA KUONYESHWA KADI NYEKUNDU MCHEZAJI HUYO BAADHI YA
WACHEZAJI WA YANGA HAWAKUKUBALIANA NA ADHABU HIYO NA KUANZISHA VURUGU KWA
MWAMUZI ISRAEL
NKONGO NA HATA KUDIRIKI KUMPIGA. KATIKA TUKIO HILO LA KUMPIGA MWAMUZI WACHEZAJI
WENGINE WALIPEWA KADI NYEKUNDU NA
KUISABABISHIA TIMU YAO KUENDELEA NA MCHEZO WAKIWA NA WACHEZAJI PUNGUFU.
KUTOKANA NA TUKIO HILO CHAMA CHAMA CHA WAAMUZI NCHINI FRAT
KINALAANI KWA NGUVU ZOTE VITENDO VYA VURUGU VILIVYOFANYWA NA BAADHI YA
WACHEZAJI WA YANGA KWA VILE VITENDO HIVYO SI VYA KIUANAMICHEZO HASA KATIKA
MCHEZO WA MPIRA WA MIGUU, MCHEZO UNAOCHEZWA KWA KUFUATA SHERIA NA KANUNI ZA
MASHINDANO HUSIKA, NA KUWATAKA WACHEZAJI WOTE NCHINI KUTOFANYA KAMA
WALIVYOFANYA BAADHI YA WACHEZAJI WA YANGA, KWANI WACHEZAJI HAO WAMEIPAKA MATOPE
TIMU YA YANGA KWANI VITENDO HIVYO SI SEHEMU YA HISTORIA BORA YA WACHEZAJI WA
TIMU YA YANGA.
AIDHA, FRAT INATOA PONGEZI ZA DHATI KWA KAPTENI WA TIMU YA
YANGA NA TIMU YA TAIFA SHADRAK MSAJIGWA KWA KUONYESHA UKOMAVU KAMA KAPTENI KWA
KUWAZUIA WACHEZAJI WAKE KUTENDA YALE WALIYOKUWA WANAKUSUDIA KUYATENDA PIA
KAPTENI HUYO AMENUKULIWA NA VYOMBO VYA HABARI AKIKEMEA VITENDO VILIVYOFANYWA NA
BAADHI YA WACHEZAJI WENZAKE.
PIA FRAT INAMPONGEZA KOCHA MKUU WA TIMU YA YANGA KOSTADIN
PAPIC KWA KUKEMEA VITENDO VYA WACHEZAJI WAKE NA KUIKEMEA NIDHAMU MBOVU
ILIYOONYESHWA NA BAADHI YA WACHEZAJI WA TIMU YAKE.
PIA TUNAWAPONGEZA WACHEZAJI WOTE NA DAKTARI WA TIMU YA
YANGA,AMBAO KWA NAMNA MOJA WALIJARIBU KWA NGUVU ZOTE KUWAZUIA WACHEZAJI
WALIOKUWA NA HALI YA KUMPIGA MWAMUZI WA MCHEZO HUO.
VURUGU HIZO ZIMEKEMEWA NA VIONGOZI WA SERIKALI, RAIS WA
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU NCHINI NA WALE WOTE WANAOPENDA MAENDELEO YA MCHEZO
HUO HAPA NCHINI.
CHAMA CHETU KINAUNGA MKONO KWA DHATI KAULI ILIYOTOLEWA NA
RAIS WA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU NCHINI KWA KUKEMEA VITENDO AMBAVYO
HAVIKUZI MAENDELEO YA SOKA HAPA NCHINI BALI VINADUMAZA NA KUTUWEKA KATIKA SURA
MBAYA KWA WADAU MBALIMBALI WA MCHEZO WA SOKA IKIWA NI PAMOJA NA KUFANYIKA KWA
UHARIBIFU WA MALI ZA SERIKALI NA WATU BINAFSI BILA SABABU ZA MSINGI ZA
KUHALALISHA MATENDO HAYO.
VITENDO VYA WACHEZAJI HAO VILIWAHI KUTOKEA MIAKA YA AROBAINI
NA SABA KATIKA LIGI NDOGO NA SI KWENYE LIGI
KUU NCHINI. KWA HIYO WALE WOTE WALIOFANYA VITENDO HIVYO WANAWAJIBIKA KUWAOMBA
RADHI WATANZANIA KWA VITENDO VYAO AMBAVYO VIMETENGENEZA HISTORIA MBAYA KATIKA LIGI KUU HAPA NCHINI.
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU HAPA NCHINI LIMEWEKA KANUNI NA TARATIBU AMBAZO KAMA TIMU
HAIKURIDHIKA NA YALE YANAYOJITOKEZA KWENYE MCHEZO, ZITATAKIWA KUZIFUATA ILI KUDAI HAKI ZAO NA SI
VINGINEVYO.
NI IMANI YETU KWAMBA MAFUNZO TULIYOYAPATA KUTOKANA NA TUKIO HILO YATABAKI KUWA SEHEMU
YA HISTORIA NA KUTORUDIWA TENA NA TIMU YOYOTE. TIMU YA YANGA NI MIONGONI MWA
TIMU KUBWA HAPA NCHINI AMBAPO WACHEZAJI, VIONGOZI NA WAPENZI WAKE WANAPASHWA
KUWA MFANO BORA WA KUIGWA NA HILO LINAWEZEKANA ENDAPO KUTAKUWA NA UTASHI WA
DHATI WA KUJENGA TIMU BORA NA YENYE KUHESHIMIWA TANZANIA NA NJE YA TANZANIA.
MCHEZAJI MWASIKA MMOJA KATI YA WACHEZAJI WALIOSHIRIKI
KUMPIGA MWAMUZI AMENIPIGIA SIMU AKINIOMBA RADHI MIMI NA WAAMUZI WOTE KWA UJUMLA NA KUNIOMBA
NIMSAIDIE KUMUOMBEA MSAMAHA KWA MWAMUZI WA MCHEZO HUO LAKINI HIYO
HAITOSHI;NAMSHAURI MCHEZAJI HUYO AJITOKEZE HADHARANI ASIOMBE RADHI KWA SIRI
KWANI WALIOATHIRIKA SIKU ILE SI NKONGO PEKE YAKE NI PAMOJA NA WATU WENGINE
AMBAO WALIKUJA KUONA MCHEZO WA SOKA NA SI MASUMBWI, NAAMINI MWASIKA ANAJUTIA
MAKOSA YAKE NA NI MUUNGWANA, ATAJITOKEZA KUOMBA RADHI HADHARANI ILI AWE SEHEMU YA JAMII INAYOPENDA MAMBO
MEMA.
MWISHO NAOMBA VIONGOZI WA YANGA, WAPENZI NA WACHEZAJI,KWAMBA
HUU SI WAKATI WA KULUMBANA KWA YALIYOTOKEA BALI NI WAKATI WA KUJISAHIHISHA ILI
AIBU ILE ISITOKEE TENA; TUSIPOKEMEA YALE YALIYOJITOKEZA JANA KWENYE UWANJA WA
TAIFA KESHO TUTAFANYA VILE VILE KWENYE NCHI ZA WATU, ITAKUWA NI AIBU KWA TAIFA
NA SI YANGA PEKEE NA HIYO SI HULUKA YA WATANZANIA.
MICHEZO NI FURAHA, UPENDO, UNDUGU, MSHIKAMANO NA KUSHINDANA.
LESLIE L LIUNDA
KARIBU MKUU
FRAT TAIFA
Comments
Post a Comment