Daktari wa timu ya Bolton Wonderers Jonathan Tobin ameelezwa kwamba nyota wa timu hiyo Fabrice Muamba alikuwa mfu kwa zaidi ya dakika 78, kutokana na ugonjwa wa Moyo ambao ulisabababisha lililomdondosha uwanjani mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kutokana na hali hiyo Muamba alikimbizwa katika hospitali ya London Chest na kulazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), huku madaktari wakisema ni mapema sana kubaini kama nyota huyo ataweza kucheza tena soka.
Hata hivyo Dk. Tobin
amesema kuwa marejeo ya fahamu aliyoyapata kiungo huyo mwenye miaka 23
yanamjaza matumaini ya kupona haraka. "Tulijawa hofu kubwa mno na hatukufikiria kwa wakati huo kwamba
angerejea katika hali ya kawaida. Ilikuwa ni ajabu mno."
Muamba alipata janga la moyo
dakika ya 40, wakati akiichezea Bolton mechi ya Kombe la FA dhidi ya Tottenham
Hotspur kwenye uwanja wa White Hart Lane Jumamosi na kukimbizwa London Chest
kwa matibabu zaidi.
Comments
Post a Comment