Mechi namba 146 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Mtibwa Sugar
na Simba iliyochezwa Machi 18 mwaka huu Uwanja wa Jamhuri, Morogoro imeingiza
sh. 31,230,000.
Jumla ya watazamaji 10,410 walikata tiketi kushuhudia mechi
hiyo kwa kiingilio cha sh. 3,000. Baada ya kuondoa gharama za awali za mchezo
na asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ambayo ni sh. 4,763,898.31
kila timu ilipata sh. 6,508,230.51, uwanja sh. 2,169,410.17.
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA) sh.
867,764.07, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 2,169,410.17,
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,084,705.08, Baraza la Michezo
la Taifa (BMT) sh. 216,941.02 na asilimia 10 ya gharama za mechi sh.
2,169,410.17.
Gharama za awali za mechi zilikuwa nauli ya ndani kwa
waamuzi sh. 10,000, nauli ya ndani kwa kamishna wa mchezo sh. 10,000. mwamuzi
wa akiba sh. 30,000, posho ya kujikimu kwa waamuzi sh. 120,000 na tiketi sh.
2,480,000.
Gharama nyingine ni Jichangie ambayo ni sh. 200 kwa kila
tiketi; kila klabu ilipata sh. 728,700 wakati Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa
Morogoro (MRFA) kilipata sh. 624,600.
VILLA, JKT KUHITIMISHA RAUNDI YA 21 MACHI 21
Mzunguko wa 21 wa Ligi Kuu ya Vodacom unakamilika Machi 21
mwaka huu kwa mechi namba 147 kati ya Villa Squad na JKT Ruvu itakayochezwa
Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam .
Machi 24 mwaka huu kutakuwa na mechi ya ligi hiyo kati ya
Moro United na African Lyon. Mechi hiyo namba 149 itafanyika Uwanja wa Chamazi,
Dar es Salaam .
Mechi za Machi 28 mwaka huu ni Ruvu Shooting Stars
itakayocheza na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi wakati
Moro United itakuwa mwenyeji wa Villa Squad katika mechi namba 153
itakayofanyika Uwanja wa Chamazi, Dar
es Salaam .
Comments
Post a Comment