WIMBO ‘Mpenzi
Chocolate’, ulioimbwa na kundi la muziki wa mipasho la Jahazi Modern
Taarab, la jijini Dar es Salaam chini ya Mfalme Mzee Yusuf, umekuwa kiburudisho cha nguvu kwa
wachezaji wa timu ya Es Setif ya Algeria.
Katika kuthibitisha kuwa
wimbo huo unawaliza wachezaji hao walimuomba dereva wa gari linalowabeba aina
ya Nissan Civilian min Bus na T 413 BXN, kuwawekea wimbo huo wakati wakitoka
kwenye mazoezi ya leo asubuhi kwenye uwanja wa Karume.
Mara baada ya dereva huyo
kuwawekea wimbo huo wenye wachezaji hao walianza kupiga mbinja na makofi
wakishangilia jambo lililoonesha kuwa wimbo huo umewakuna vilivyo.
“Hawa wachezaji hata wakati
wakija hapa uwanjani asubuhi walikuwa wakipiga makofi huku wakishangilia wimbo
wa taarbu uliokuwa ukipigwa kwenye gari lao lakini mimi sikuusikia wimbo
wenyewe,” alisema mmoja wa mashuhuda.
Comments
Post a Comment