MAUTI YA MKUTA UWANJANI NYOTA WA SOKA

NYOTA wa soka nchini India, amefariki dunia baada ya kupatwa na ugonjwa wa moyo akiwa katika mechi ya Ligi ya Shirikisho la Soka la India ngazi ya Wilaya ya Bangalore, Kusini mwa Jiji la Bangalore.
Aliyefariki dunia ni kiungo D. Venkatesh, 27, wa Bangalore Mars, ambaye aliingia akitokea benchi dakika ya 73 na kudondoka mwishoni mwa mechi hiyo, dhidi ya klabu ya South Western Railway.
Vyombo vya habari nchini India vimeripoti leo kuwa wakati mechi hiyo ikichezwa kulikuwa hakuna gari la wagonjwa uwanjani hapo na Venkatesh alifikishwa katika Hospitali ya Hosmat kwa kutumia baiskeli ya matairi matatu ‘Guta’.
Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa sababu za kifo cha nyota huyo ni ugonjwa wa moyo.
Gazeti la The Times nchini India, lilimkariri Dk. Ajith Benedict Royan wa Hospitali ya Hosmat, akisema kuwa hakukuwa na majeraha yoyote ya nje yalioonekana katika mwisli wa Venkatesh, yanayoweza kuwa kama sababu ya kifo cha ghafla cha mchezaji huyo.
“Labda kama angetundikiwa oksijeni au matibabu sahihi wakati wa tukio, ingesaidia kuokoa  moyo kusimama,” gazeti hilo lilimkariri Royan akisema.

Shirikisho la Soka la India kwa ngazi zote (AIFF) limethibitisha kutokea kwa kifo cha mchezaji huyo na katika maelezo yake kikasema: “AIFF inamuombea Venkatesh apumzike kwa amani.”

Comments