KAMATI YA UTENDAJI TFF YAKUTANA LEO



KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inatarajiwa kukutana kesho kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ajenda kuu ikiwa ni kuhusu Mkutano Mkuu wa mwaka uliokwama kufanyika mwaka jana kwa mujibu wa katiba na sasa utafanyika Machi 24.
TFF ilishindwa kufanya Mkutano mwaka jana bila ya sababu za msingi na sasa watalazimika kuwa na bajeti pana mwaka huu kufanya mikutano miwili mikubwa, kwanza huu wa mwsihoni mwa mwezki na baadatye mwishoni mwa mwaka watakuwa na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi.
Chanzo chetu cha habari kutoka TFF, kimesema kwamba katika Mkutano wa kesho Wajumbe watalazimika kufanya 'fasta' ili jioni waweze kushuhudia mechi ya Ligi Kuu, kati ya Yanga na Azam Uwanja wa Taifa. 

Comments