UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya kutakatisha
fedha haramu inayomkabili Msanii wa Filamu nchini, Kajala Masanja na mumewe
Faraja Chambo jana ulishindwa kuleta hati ya mashtaka iliyofanyiwa marekebisho
kama ulivyoamriwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wiki
iliyopita kwa madai kuwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Dk. Eliezer Feleshi juzi
hakuweza kupatikana ofisini kwake ili aweze kutoa kibali.
Wakili wa Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mussa Hussein, aliikumbusha mahakama hiyo kuwa, kesi hiyo
jana ilikuja kwa ajili ya upande wa jamhuri kuleta hati ya mashtaka
iliyofanyiwa marekebisho, lakini ameshindwa kufanya hivyo kwa sababu juzi, DDP Dk.
Feleshi hakuwepo ofisini kwake ili aweze kutoa kibali cha kuletwa hati hiyo
mahakamani, kwa hiyo wanaomba wapewe siku moja waweze kutekeleza hilo.
Kwa upande wake,
Hakimu Mkazi Sundi Fimbo, alikataa hati hiyo isiletwe leo na badala yake, hati
hiyo iletwe Machi 26 mwaka huu kwa ajili wa washtakiwa kusomewa upya mashtaka
hayo na akaamuru mshtakiwa arudishwe rumande, uamuzi ambao ulikubaliwa na
wakili huyo wa Takukuru na wakili wa Kajala, Alex Mgongolwa.
Machi 15 mwaka huu,
Kajala na mumewe, ambaye pia yupo gerezani anakabiliwa na kosa la utakatishaji
fedha haramu katika kesi nyingine, ambako kwa mujibu wa sheria, kosa hilo halina dhamana.
Comments
Post a Comment