UONGOZI wa Chama cha Soka
Mkoa wa Dar es Salaam
(DRFA), kesho unatarajia kukutana na viongozi wa klabu zote za mkoa huo kwa
lengo la kujadili mwanzo wa Ligi ya Kanda ya Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa chama hicho, Amin Bakhressa, alisema mkutano huo utafanyika
katika ukumbi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuanzia saa tisa alasiri.
Alisema mkutano huo
utatoa fursa kwa klabu kujadiliana kwa kina juu ya uendeshaji wa ligi hiyo,
ambapo kila timu inatakiwa kuwakilishwa na kiongozi mmoja, huku makatibu wakuu
wa vyama vya soka wilaya ya Kinondoni, Temeke na Ilala nao wakiwakilisha wilaya
zao katika mkutano huo.
“Viongozi hao wanatakiwa
kufika kwenye mkutano wakiwa na usajili wa wachezaji wao, na baada ya mkutano
kumalizika, kutakuwa na uhakika wa kuanza ligi yetu mapema,” alisema Bakhressa.
Ligi hiyo itatoa timu
tatu kwa ajili ya kuwakilisha mkoa wa Dar
es Salaam kushiriki Ligi ya Taifa.
Pia Bakhressa alitoa
mwito kwa timu zilizofuzu kushiriki ligi hiyo kulipa mapema ada ya ushiriki sh
75,000, ili kuthibitisha uwapo wao mashindanoni.
Comments
Post a Comment