BEKI
wa kati wa Manchester United, Mserbia Nemanja Vidic, amekana taarifa za
uwezekano wa kurudi dimbani msimu huu na kuwataka mashabiki wake na wa klabu
kumsubiri hadi msimu ujao anakotarajia kuanzia katika mechi za maandalizi ya
msimu ‘Pre-Season’.
Ripoti
za mwanzini mwa wiki hii zilidai kuwa Nemanja ambaye yuko nje ya dimba tangu mwezi
Desemba 2011, alikuwa mbioni kurudi katika mechi ya mahasimu wa Jiji la
Manchester, City na United itakayopigwa Aprili 30 kwenye dimba la Etihad.
Hata hivyo Vidic amezikana taarifa hizo na kusisitiza anaweza kuwa tayari kwa kuchezea
United angalau hadi mwezi Julai, wakati klabu hiyo itakapokuwa kwenye mechi za
maandalizi ya msimu huko Mashariki ya Mbali.
“Uponaji
wangu unakwenda vema na ninatarajia kuanza mazoezi tena mwezi Julai mwaka huu.
Nafanya kazi ya ziada hivi sasa. Mtarajio ni kwamba ninaweza kurejea dimbani
kwa ajili ya msimu ujao.”
Comments
Post a Comment