Msanii Mkongwe wa bendi Kwongwe ya Msondo Ngoma Music,Muhidini Gurumo
akiwa
katika hospital ya Taifa Muhimbili, Dar es salaam jana, akipimwa
mapigo ya
Moyo na Ofisa Muuguzi Msaidizi wa Hospital hiyo,Suraiya
Mohamed alipolazwa
kufanyiwa uchunguzi wa kina toka mwishoni mwa wiki
iliyopita.(Picha na
www.burudan.blogspot.com)
Na Mwandishi Wetu
MWANAMUZIKI
maarufu wa bendi kongwe ya Msondo ngoma, Muhidin Gurumo
aliyelazwa Hospitali
ya Taifa ya Muhimbili kwa ugojwa wa shinikizo la
damu anaendelea
vizuri.
Akizungumza na Dar es Salaam jana,Msemaji wa bendi hiyo
Rajabu Mhamila
'Super 'D' alisema Afya ya Gurumo inaendelea vizuri na wakati
wowote
anaweza kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.
Alisema kuwa
madaktari wanataka kuchukua vipimo vya mwisho kwa kina
kujua kila kitu
kinachop msumbua katika mwili wake.
"Kwa sasa tunashukuru Mungu afya ya
Gurumo inaendelea vizuri tofauti
na mara ya kwanza na akiendelea hivi anaweza
hakurusiwa hivi
karibuni"alisema Super D.
Hata hivyo aliwataka wapenzi
wa bendi hiyo kumuombea duwa mwanamziki
huyo ili apone upesi pia aliongeza
kwa kusema maonesho yao ya wikii
hii ni kama ifuatavyo Alhamisi watakuwa
Mwandege Mkoa wa Pwani,Ijumaa
watapiga katika viwanja vya Lidaz Clab jumamosi
watakuwa katika
viwanja vya TCC Sigara na Jumapili watamaliza wiki endi
katika ukumbi
wa Max Bar uliopo Ilala Bungoni alisema Super D.
Comments
Post a Comment