YANGA WAENDA MISRI BILA BERKO, GUMBO


MSAFARA wa Yanga utaondoka alfajir ya kesho kwenda Cairo Misri tayari kwa mechi yake ya marudiano ya ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Zamalek ya huko utakaopigwa Machi 4.
Hata hivyo katika msafara huo watakosekana nyota wake kadhaa wakiwemo kipa Mghana Yaw Berko na Rashid Gumbo.
Wachezaji watakaoondoka ni pamoja na Shaban Kado, Shadrack Nsajigwa, Athuman Iddy ‘Chuji’, Juma Seif, Nurdin Bakari, Chacha Marwa, Godfrey Taita, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Omega Seme, Davies Mwape, Pius Kisambale, Hamis Nombo, Oscar Joshua, Haruna Niyonzima, Jerry Tegete, Job Ibrahim, Stefano Mwasyika, Kenneth Assamoh na  Shamte Ally.

Comments